PlaneteAfrique
Déconnexion
WS-Apps, le système de gestion de contenus adaptatif développé depuis 15 ans, conçu pour sa puissance, son efficacité et sa simplicité. Trois applications, une présence web maîtrisée :
WS-MySite! Votre présence web immédiate et professionnelle. Découvrir ce pack
WS-Webzine Pour agences de presse et éditeurs. Découvrir ce pack
WS-Ecommerce Vendez en ligne et encaissez par Mobile Money et carte bancaire. Découvrir ce pack

Watuhumiwa wa ukataji mkono wa albino wafikishwa mahakamani

Watuhumiwa wa ukataji mkono wa albino wafikishwa mahakamani


Watuhumiwa watano wanaodaiwa kushiriki katika kitendo cha kumkata mkono Mlemavu wa ngozi Albino Maria Chambanenje wa kijiji cha Miangalua wilayani Sumbawanga wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu mkazi wilayani Sumbawanga kusomewa mashtaka yao.



Watuhumiwa  hao  wamefikishwa  mahakamani  baada  ya uchunguzi wa  jeshi  la  polisi  kubaini  walikuwa  na  mkono wa  Albino  huyo ambao walifukia ardhini   mara baada  ya kuukata. 



Watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali wa askari Polisi na kusomewa mashtaka yao huku wakitakiwa kutojibu lolote, ambapo upande wa Jamhuri ukiwashtaki kwa  makosa mawili ikiwa ni pamoja na kosa la kula njama ya kutaka kuua  na kujaribu kuua.



Miongoni mwa washtakiwa hao yupo Mume wa Albino huyo Gabriel Yohana, shemeji yake Gaudensi Yohana, Mganga wa jadi Kaponda Muyamba, Mtuhumiwa wa kutengeneza mchoro huo Linus Silukala na Mtuhumiwa aliyetaka kuununua mkono huo Mtogwa Cosmas alimaarufu kama mzee wa Ishu mkazi wa Sokomatola jijini Mbeya.



Hatahivyo mahakama hiyo iliyokuwa chini ya Hakimu mkazi Mh. Rosalia Mugisa imeweka wazi dhamana kwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja huku mahakama hiyo ikitoa masharti manne ya dhamana hiyo, ikiwa ni pamoja na kuwa na wadhamini watatu wakazi wa wilayani Sumbawanga, fedha taslimu shilingi milioni tatu kila mmoja, na mmoja wa wadhamini awe ni mwajiriwa wa serikali au Shirika lolote la umma, ambapo washtakiwa hao walishindwa maaelekezo ya dhamana hiyo na kurudishwa mahabusu hadi Machi sita itakapotajwa tena.



Adolph Mbata, TBC Sumbawanga.




Last Updated ( Friday, 22 February 2013 11:23 )


 


TANZANIE - accès rapides

Actualités par pays

 

Newsletter


 
 
 
 
 
 

Actualités par pays

Newsletter


 
 
 
 
 
Tanzanie - Actualites